dcsimg

Fungo (familia) ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Fungo, paka-zabadi au paka wa zabadi ni wanyama mbua wa ukubwa mdogo hadi wastani katika familia Viverridae. Spishi nyingine huitwa kanu, oyani na binturongi, lakini fungo-miti wa Afrika hana mnasaba sana na fungo na yumo katika familia yake binafsi Nandiniidae. Fungo wanatokea Afrika, Asia na Rasi ya Iberia katika maeneo kama savana, milima na misitu, hususa misitu ya mvua. Hawa ni miongoni mwa wanyama wa asili wa oda Carnivora. Mifupa yao ni takriban sawa na ile ya visukuku vya Eocene hapo ilikuwa miaka milioni 50. Wanafanana na paka wenye pua ndefu na mkia mrefu. Wana kucha zinazoweza kurudiwa ndani, mfupa katika mboo wao na tezi za harufu kando ya mkundu. Ukubwa wao unatofautiana kutoka ule wa oyani (mwili wa sm 30 na uzito wa g 650) hadi fungo wa Afrika (sm 84 na kg 18), lakini binturongi anaweza kuwa kg 25.

Fungo hukiakia usiku na kwa hivyo wana uwezo mzuri sana wa kusikia na kuona, lakini spishi nyingi huonekana mchana pia. Kinyume na uainisho wao katika oda Carnivora wanyama hawa hula vitu vyingi na fungo-miti ni walamimea takriban kabisa. Kwa hivyo chonge zao (meno yaliyochongoka ambayo yatumika kwa kunyafua nyama) zimevia. Kinyaa cha tezi za harufu kinaitwa zabadi na hutumika kwa kuchanganya katika manukato. Angalau zabadi inatengenezwa kwa jinsi ya kikemia sikuhizi, inavunwa kutoka wanyama hata sasa. Katika Afrika fungo hutumika, hususa huko Uhabeshi.

Uainishaji

Picha

Marejeo

  1. 1.0 1.1 1.2 "The taxonomy of the endemic golden palm civet of Sri Lanka". Zoological Journal of the Linnean Society (The Linnean Society of London) (155): 238–251. 2009. .

Viungo vya nje

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Fungo (familia): Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Fungo, paka-zabadi au paka wa zabadi ni wanyama mbua wa ukubwa mdogo hadi wastani katika familia Viverridae. Spishi nyingine huitwa kanu, oyani na binturongi, lakini fungo-miti wa Afrika hana mnasaba sana na fungo na yumo katika familia yake binafsi Nandiniidae. Fungo wanatokea Afrika, Asia na Rasi ya Iberia katika maeneo kama savana, milima na misitu, hususa misitu ya mvua. Hawa ni miongoni mwa wanyama wa asili wa oda Carnivora. Mifupa yao ni takriban sawa na ile ya visukuku vya Eocene hapo ilikuwa miaka milioni 50. Wanafanana na paka wenye pua ndefu na mkia mrefu. Wana kucha zinazoweza kurudiwa ndani, mfupa katika mboo wao na tezi za harufu kando ya mkundu. Ukubwa wao unatofautiana kutoka ule wa oyani (mwili wa sm 30 na uzito wa g 650) hadi fungo wa Afrika (sm 84 na kg 18), lakini binturongi anaweza kuwa kg 25.

Fungo hukiakia usiku na kwa hivyo wana uwezo mzuri sana wa kusikia na kuona, lakini spishi nyingi huonekana mchana pia. Kinyume na uainisho wao katika oda Carnivora wanyama hawa hula vitu vyingi na fungo-miti ni walamimea takriban kabisa. Kwa hivyo chonge zao (meno yaliyochongoka ambayo yatumika kwa kunyafua nyama) zimevia. Kinyaa cha tezi za harufu kinaitwa zabadi na hutumika kwa kuchanganya katika manukato. Angalau zabadi inatengenezwa kwa jinsi ya kikemia sikuhizi, inavunwa kutoka wanyama hata sasa. Katika Afrika fungo hutumika, hususa huko Uhabeshi.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri