dcsimg

Dagaa ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Dagaa ni jina la kawaida la samaki wa oda Clupeiformes isipokuwa spishi za familia Chirocentridae. Spishi nyingi zina majina mengine pia, kama vile kapenta, kerenge, lumbu, mbarata, mwatiko, ndakala, pata, pawali, simu, uono na usipa. Spishi kadhaa za familia Alestidae, Apogonidae, Atherinidae, Cyprinidae na Leiognathidae huitwa dagaa pia lakini majina mengine yanapendelewa. Dagaa wanatokea katika bahari zote za dunia na katika maziwa na mito mingi.

Kibofuhewa cha Clupeiformes kimeungana na utumbo kwa kifereji. Kwa kawaida hawana mrabafahamu (mstari wa ubavu, lateral line kwa Kiingereza) lakini wana macho, mapezi na magamba ambayo ni ya kawaida kwa samaki wengi, ingawa siyo samaki wote wana sifa hizi. Wao ni samaki wenye rangi ya fedha na mwili mwembamba wenye umbo la dulabu, na mara nyingi huunda makundi. Takriban spishi zote hula planktoni ambazo huzichuja kutoka kwa maji kwa matamvua yao.

Spishi zilizochaguliwa za Afrika ya Mashariki

Picha

Marejeo

  • Rashid Anam & Edoardo Mostarda (2012) Field identification guide for the living marine resources of Kenya. FAO, Rome.
  • Gabriella Bianchi (1985) Field guide to the commercial marine brackish-water species of Tanzania. FAO, Rome.

Viungo vya nje

Dagaa kwenye hifadhidata ya samaki

Crystal Clear app babelfish vector.svg Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Dagaa kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Dagaa: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Dagaa ni jina la kawaida la samaki wa oda Clupeiformes isipokuwa spishi za familia Chirocentridae. Spishi nyingi zina majina mengine pia, kama vile kapenta, kerenge, lumbu, mbarata, mwatiko, ndakala, pata, pawali, simu, uono na usipa. Spishi kadhaa za familia Alestidae, Apogonidae, Atherinidae, Cyprinidae na Leiognathidae huitwa dagaa pia lakini majina mengine yanapendelewa. Dagaa wanatokea katika bahari zote za dunia na katika maziwa na mito mingi.

Kibofuhewa cha Clupeiformes kimeungana na utumbo kwa kifereji. Kwa kawaida hawana mrabafahamu (mstari wa ubavu, lateral line kwa Kiingereza) lakini wana macho, mapezi na magamba ambayo ni ya kawaida kwa samaki wengi, ingawa siyo samaki wote wana sifa hizi. Wao ni samaki wenye rangi ya fedha na mwili mwembamba wenye umbo la dulabu, na mara nyingi huunda makundi. Takriban spishi zote hula planktoni ambazo huzichuja kutoka kwa maji kwa matamvua yao.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri