dcsimg

Nzi ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Nzi ni wadudu wadogo wa nusuoda Brachycera katika oda Diptera (yaani “wenye mabawa mawili”). Kwa asili jina hili limetumika kwa wadudu wa familia Muscidae, lakini kwa sababu spishi nyingi za Brachycera hazina majina ya Kiswahili, “nzi” linapendekezwa kama jina kwa Brachycera wote. Nusuoda nyingine ya Diptera, Nematocera, inashirikisha mbu na jamaa wao.

Diptera wote wana mabawa mawili tu yaliyopo kwa mesotoraksi. Mabawa ya nyuma ya asili yamepunguzika na kubadilika kuwa virungu (halteres) ambavyo vinasaidia mdudu ajue mkao wake na mabadiliko ya mwelekeo (kama aina ya gurudumu tuzi). Vipapasio vya Brachycera ni vifupi na vina mapingili machache kuliko Nematocera, mara nyingi matatu tu lakini hadi 7. Spishi nyingi zinabeba unywele (arista) juu ya pingili la tatu la vipapasio. Nzi hawana sehemu za kinywa zinazoweza kutumika kwa kutafuna, kwa hivyo hula chakula cha majimaji au cha chembe ndogo (kama chavua).

Lava wa nzi hawana miguu na wanafanana na minyoo. Kwa kawaida wana meno mawili yaliyopindika (kama kulabu) na spirakulo mbili kwenye nyuma ya kiwiliwili. Huonekana mara nyingi katika nyama iliyooza na katika matunda.

Spishi kadhaa za Afrika

Picha

Blue morpho butterfly.jpg Makala hii kuhusu mdudu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nzi kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri

Nzi: Brief Summary ( Swahili )

provided by wikipedia emerging languages

Nzi ni wadudu wadogo wa nusuoda Brachycera katika oda Diptera (yaani “wenye mabawa mawili”). Kwa asili jina hili limetumika kwa wadudu wa familia Muscidae, lakini kwa sababu spishi nyingi za Brachycera hazina majina ya Kiswahili, “nzi” linapendekezwa kama jina kwa Brachycera wote. Nusuoda nyingine ya Diptera, Nematocera, inashirikisha mbu na jamaa wao.

Diptera wote wana mabawa mawili tu yaliyopo kwa mesotoraksi. Mabawa ya nyuma ya asili yamepunguzika na kubadilika kuwa virungu (halteres) ambavyo vinasaidia mdudu ajue mkao wake na mabadiliko ya mwelekeo (kama aina ya gurudumu tuzi). Vipapasio vya Brachycera ni vifupi na vina mapingili machache kuliko Nematocera, mara nyingi matatu tu lakini hadi 7. Spishi nyingi zinabeba unywele (arista) juu ya pingili la tatu la vipapasio. Nzi hawana sehemu za kinywa zinazoweza kutumika kwa kutafuna, kwa hivyo hula chakula cha majimaji au cha chembe ndogo (kama chavua).

Lava wa nzi hawana miguu na wanafanana na minyoo. Kwa kawaida wana meno mawili yaliyopindika (kama kulabu) na spirakulo mbili kwenye nyuma ya kiwiliwili. Huonekana mara nyingi katika nyama iliyooza na katika matunda.

license
cc-by-sa-3.0
copyright
Waandishi wa Wikipedia na wahariri